(Go: >> BACK << -|- >> HOME <<)

Nenda kwa yaliyomo

Fred Astaire

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Fred mnamo 1941 katika seti ya filamu ya You'll Never Get Rich.

Fred Astaire alizaliwa kama Frederick Austerlitz mnamo Mei 10, 1899 mjini Omaha, Nebraska kisha akafariki Juni 22, 1987 huko mjini Los Angeles, California.

Astaire alikuwa mwigizaji, mwanamuziki, mwimbaji, na hasa mchezaji wa densi maarufu, anayejulikana kwa uwezo wake wa kipekee wa kucheza densi na kufanya miondoko ya kuvutia kwenye filamu na maonyesho ya muziki. Alianza kazi yake ya sanaa akiwa kijalunga, akishirikiana na dada yake Adele katika maonyesho ya muziki ya vaudeville.

Baada ya dada yake kustaafu, Fred aliendelea na kazi ya filamu. Akaja kuwa mmoja wa nyota wakubwa wa Hollywood. Filamu zake za densi, hasa zile alizoshirikiana na Ginger Rogers, zilimletea umaarufu wa kutosha. Filamu walizocheza pamoja ni "Top Hat" (1935), "Swing Time" (1936) na "Shall We Dance" (1937). Mtindo wao wa kipekee ulizaa kemia ya kuvutia sinemani.

Fred Astaire pia aliigiza katika filamu nyingine maarufu kama "Holiday Inn" (1942) ambapo alicheza pamoja na Bing Crosby, na "Easter Parade" (1948) akiwa na Judy Garland. Alionyesha umahiri wake wa densi na uimbaji katika filamu hizi, akileta burudani ya hali ya juu kwa watazamaji.

Viungo vya Nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Fred Astaire kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.